Abiria 35wanusurika kifo katika basi la MBAZI
Takribani abiria Thelathini na Watano wamenusurika kifo baada ya basi la kampuni ya MBAZI walilokuwa wakisafiria kutoka mkoani ARUSHA...
https://zindukaleo.blogspot.com/2014/11/abiria-35wanusurika-kifo-katika-basi-la.html
Takribani abiria Thelathini na Watano wamenusurika kifo baada ya basi la kampuni ya MBAZI walilokuwa wakisafiria kutoka mkoani ARUSHA kuelekea jijini DAR ES SALAAM kuacha njia katika eneo la MWANGA Mjini mkoani KILIMANJARO.
Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya simu, Mkuu wa wilaya ya MWANGA SHAIBU NDEMANGA amesema majeruhi Saba wa ajali hiyo hali zao sio nzuri na wamelazwa chumba cha uangalizi katika hospitali ya KCMC.
Amesema majeruhi wengine ishirini na Wanane wanapatiwa matibabu katika kituo cha afya cha wilaya ya MWANGA.

