Mswada wa sheria ya dawa za kulevya kuwasilishwa bungeni
WILLIAM LUKUVI Serikali inatarajia kuwasilisha bungeni Muswada wa Sheria mpya ya ...
https://zindukaleo.blogspot.com/2014/11/mswada-wa-sheria-ya-dawa-za-kulevya.html
Akizungumza na vyombo vya habari mjini Dodoma, Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge WILLIAM LUKUVI amesema Sheria hiyo itaondoa changamoto zilizokuwa zikijitokeza wakati wa matumizi ya sheria iliyopo sasa.
Taarifa ya hali ya dawa za kulevya nchini ya mwaka 2013 inaonesha pamoja na mambo mengine mafanikio katika udhibiti wa dawa za kulevya katika kipindi cha mwaka 2013 ikilinganishwa na miaka iliyotangulia ambapo idadi ya watuhumiwa ilipungua kutoka 6,215 mwaka 2006 hadi watuhumiwa 1,547 mwaka 2013.

